Monday, October 22, 2012

BIASHARA NDOGONDOGO.



Tanzania ni nchi mojawapo katika nchi tatu zinazoongoza kwa kasi ya kukua,kutokana na takwimu za vyama vya kimataifa.Na pia kutokana na takwimu hizo pia zinaonyesha uchumi wa bara la afrika unakua kwa kasi zaidi kuliko mabara mengine.

thumekua tukishuhudia watanzania wengi sasa wakijihusisha na ujasiriamali kwa kuanzisha biashara ndogondogo zinazowapatia kipato.
Bwana Abubakari Fikiri (31) maarufu kwa jina la 'Fundi Abuu',amekua akijishughulisha na shughuli za ushonaji nguo kwa mwaka wa tatu sasa.Alisema kuwa,kazi hiyo inamsaidia kupata kipato anachoweza kujikimu mahitaji yake yote na familia yake,kama alivyoeleza akiwa mtoni kijichi,jijini Dar es Salaam.

Katika banda hili,huuzwa vitu vya kiasili kama vile vikapu,vikoi,michoro mbalimbali na urembo kama vile hereni na vingine vingi.Bidhaa hizi huandaliwa na wabunifu na wajasiriamali wa kikundi cha Umoja wa jijini Dar es Salaam

Bwana Selemani Idd (28),ni mjasiriamali anaeuza viazi ulaya katika soko la mtongani wilaya ya temeke, jijini Dar es Salaam.

Inafurahisha na kuleta matumaini sana kuwaona ndugu zetu hawa wa jijini Dar es Salaam walivyoamua kutumia ubunifu,ujuzi na bidii bila kukata tamaa.Hawakujali hali waliyo kua nayo na kuanzisha biashara ndogondogo kwa malengo ya kufanikiwa.Hii ni changamoto kwa watu wote,ili taifa liendelee na kukua kiuchumi ni lazima tuwe wabunifu na kujituma bila kukata tamaa katika hali yoyote.
.

No comments:

Post a Comment